Azam Fc kusaka ushindi wa kwanza CAFCC Nairobi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 21st January 2026


Azam Fc kusaka ushindi wa kwanza CAFCC Nairobi

Kikosi cha Azam FC tayari kimewasili jijini Nairobi, Kenya kuelekea mechi ya kombe la Shirikisho kundi B dhidi ya Nairobi United.

Mchezo huo utapigwa Jumapili Januari 25 kwenye Uwanja wa Taifa wa Nyayo.

Unaweza kusema ni mechi ambayo Azam Fc itaingia kwa lengo la kusaka ushindi wake wa kwanza katika michuano hiyo baada ya kupoteza mechi zote mbili zilizopita.

Wapinzani wao Nairobi United nao walipoteza mechi zote zilizopita hivyo kila mmoja ataingia kwenye mchezo huo kusaka rekodi ya ushindi wa kwanza.

Aidha matokeo tofauti na ushindi huenda yakafifisha matumaini ya Azam Fc kutinga robo fainali ya michuano hiyo licha ya kuwa na kocha mwenye uzoefu mkubwa na mashindano ya CAF, Florent Ibenge.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.