Mshambuliaji George Mpole (33) amejiunga na klab ya Tanzania Prison inayoshiriki ligi kuu ya NBC.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa vilabu vya Fc Lupopo ya Congo DR, Geita Gold na Pamba jiji amejiunga na maafande akiwa mchezaji huru.
Prisons imeendelea kuboresha kikosi chake katika dirisha hili ili kuhakikisha wanarudisha ubabe wao katika soka la Tanzania.





