Kiungo wa Simba Mzamiru Yassin amejiunga na klabu ya TRA United kwa mkopo hadi mwisho wa msimu.
Klabu ya TRA United imethibitisha usajili wa kiungo huyo punda aliyeacha alama kunako klabu ya Simba.
Mzamiru alikuwa miongoni mwa wachezaji waandamizi katika kikosi cha Simba akiwatumikia Wekundu hao wa Msimbazi wa zaidi ya misimu nane.
Tangu msimu uliopita amekuwa na wakati mgumu kupata nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha Simba na hivyo hii inaweza kuwa nafasi ya kurejesha makali yake.
Mzamiru anaungana na nyota w=mwingine wa zamani wa Simba Hassan Dilunga ambaye nae ametua TRA United akitokea klabu ya JKT Tanzania



