Kiungo wa Yanga Duke Abuya ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa ligi kuu ya NBC kwa mwezi Disemba 2025.
Abuya ameshinda tuzo hiyo mbele ya Nassor Saadun wa Azam Fc na Prince Dube wa Yanga baada ya kuhusika katika mabao mawili.
Aidha tuzo ya kocha bora imeenda kwa mkufunzi wa Yanga Pedro Goncalves ambaye aliiongoza Yanga kushinda mechi mbili.





