Local,Normal News,International,Yanga, Simba, Azam, Singida

Ligi ya mabingwa, Shirikisho mechi zimerejea

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 Jan 2026
Ligi ya mabingwa, Shirikisho mechi zimerejea

Baada ya mapumziko ya wiki kadhaa kupisha michuano ya Afcon 2025 iliyomalizika mwishoni mwa wiki iliyopita na Senegal kuibuka mabingwa, michuano ya ngazi ya klabu ligi ya mabingwa (CAFCL) na kombe la Shirikisho (CAFCC) inarejea wikiendi hii.

Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya ligi ya mabingwa, Yanga wao wako ugenini leo kumenyana na Al Ahly, mabingwa wa kihistoria wa michuano hiyo.

Mtanange huo unaosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka barani Afrika, utapigwa saa 1 usiku katika uwanja wa Borg El Arab ulio mji wa Alexandria, Misri.

Yanga iliwasili Misri usiku wa juzi ambapo vijana wa kocha Pedro Goncalves walipata siku mbili za kujiandaa na mchezo huo.

Mchezo mwingine utapigwa majira ya saa 3 usiku Mamelodi Sundowns wakiwakaribisha Al Hilal ya Sudan.

Siku ya Jumamosi wawakilishi wengine wa Tanzania (CAFCL) Simba watakuwa dimbani kule Tunis kumenyana na Esperance.

Hii ni mechi muhimu sana kwa Simba kuhakikisha haipotezi ili kuweka hai mipango ya kufuzu robo fainali.

Simba iliyo kundi D, ilianza kwa kusuasua ikipoteza mechi zote mbili za mwanzo, na sasa wanapaswa kuanza kukusanya alama.

Kwa upande wa kombe la Shirikisho (CAFCC), wawakilishi wa Tanzania katika michuano hiyo klabu za Azam Fc na Singida Black Stars zitashuka dimbani siku ya Jumapili.

Azam Fc wako ugenini Kenya kumenyana na Nairobi United wakati Singida BS watakuwa dimba la New Amaan Complex kumenyana na Otoho.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’