Klubu ya Ujerumani, Schalke 04, imethibitisha usajili wa kiungo mashambulizi mwenye uzoefu wa kimataifa, Edin Dzeko, ili kuisaidia klabu hiyo katika jitihada zake za kurudi Bundesliga. Dzeko, ambaye atasherehekea miaka 40 mwezi Machi, alihama msimu uliopita kwenda Fiorentina ya Serie A.
Hata hivyo, Dzeko ambaye amekuwa akianza michezo michache tu msimu huu kwa Fiorentina, sasa amerudi Ujerumani ili kuungana na Schalke katika lengo la kurejea kwenye ligi kuu ya Ujerumani.
Taarifa rasmi ya Schalke 04 imesema:
"FC Schalke 04 wameongeza nguvu katika safu ya mashambulizi kwa kusajili mchezaji mwenye uzoefu wa kimataifa, Edin Dzeko, kwa mechi 16 zinazosalia za msimu wa 2025/26. Mchezaji huyu ambaye ndiye mchezaji aliyecheza michezo mingi zaidi kwa Bosnia na Herzegovina, hivi karibuni alicheza Fiorentina Serie A na ni mmoja wa wafungaji bora wa kizazi chake. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 39 atavaa jezi namba 10 Schalke."
Dzeko mwenyewe ameeleza furaha yake kuungana na Schalke:
"Kutoka pale nilipoona kwamba kulikuwa na shauku kutoka Schalke, nilichunguza klabu kwa makini na kutazama mechi kadhaa. Mazungumzo yangu na klabu, na kocha mkuu Miron Muslic na, bila shaka, na Nikola Katic miongoni mwa wengine, yalikuwa chanya sana.
"Ni jambo la kuvutia kuona jinsi timu ilivyoendelea msimu huu baada ya miaka michache yenye changamoto. Sasa nataka kutoa kila kitu changu ili tufanikishe pamoja katika nusu ya pili ya msimu.
"Nina hamu kubwa ya kucheza mechi yangu ya kwanza nyumbani mbele ya mashabiki wa VELTINS-Arena wakiwa wamejaa."
Mshambuliaji huyu mwenye uzoefu alitumikia Bundesliga kwa miaka mitatu na nusu akiwa Wolfsburg kabla ya kusajiliwa na Manchester City Januari 2011.
Usajili wake Schalke unaashiria azma ya klabu hiyo kutumia uzoefu na ubora wake katika kuhakikisha inarejea Bundesliga kwa nguvu msimu huu.