International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Januari 24 2026

Joel JJ By Joel JJ
β€’
24 Jan 2026
Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Januari 24 2026

Beki wa kulia wa England, Trent Alexander-Arnold, hajaambiwa aondoke Real Madrid, licha ya ripoti kutoka Hispania kudai kuwa kocha mpya Alvaro Arbeloa amemtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 atafute klabu mpya majira haya ya kiangazi. (Mail)

Arsenal wanachunguza uwezekano wa kufanya usajili wa kiangazi kwa mshambuliaji wa Atletico Madrid na Argentina, Julian Alvarez, mwenye umri wa miaka 25. (ESPN)

Bayern Munich watakabiliwa na ushindani kutoka Liverpool katika mbio za kumsajili mshambuliaji wa Ivory Coast, Yan Diomande, 19, kutoka RB Leipzig. (Bild)

Beki wa England wa Liverpool, Joe Gomez, 28, anahitajika na AC Milan. (Calciomercato)

West Ham wamekataa ofa ya pauni milioni 32.9 pamoja na pauni milioni 3 kama nyongeza kutoka Flamengo kwa kiungo wa Brazil mwenye umri wa miaka 28, Lucas Paqueta. (The Athletic)

Kiungo wa Crystal Palace na England, Adam Wharton, 21, pamoja na kiungo wa Brighton na Cameroon, Carlos Baleba, 22, wameibuka kuwa malengo halisi zaidi kwa Manchester United kuliko kiungo wa Nottingham Forest na England, Elliot Anderson, 23, ambaye wanaamini atajiunga na Manchester City. (The I)

Liverpool wanatazamia kumrudisha beki wa kushoto wa Ugiriki, Kostas Tsimikas, 29, kutoka kwa mkopo wake Roma. (Talksport)

Chelsea wamefanya mawasiliano ya awali na Juventus kujadili dili la mkopo kwa kiungo wa Brazil mwenye umri wa miaka 27, Douglas Luiz, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo Nottingham Forest. (Fabrizio Romano)

Rennes watamlenga beki wa kati wa England wa Toulouse, Charlie Cresswell, 23, iwapo beki wa Kifaransa mwenye umri wa miaka 20, Jeremy Jacquet, ataondoka kwenda Chelsea. (Florian Plettenberg)

Brighton wamemweka wazi kuwa winga wa England mwenye umri wa miaka 19, Tommy Watson, anapatikana kwa mkopo, huku klabu kadhaa za Championship na moja ya Premier League zikionyesha nia. (Sky Sports)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
2h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
3h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
3h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
5h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
6h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
6h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
20h ago
READ MORE β†’