International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya Jumanne, Januari 27 2026

Joel JJ By Joel JJ
β€’
27 Jan 2026
Tetesi za usajili Ulaya Jumanne, Januari 27 2026

Nottingham Forest wametoa ofa ya pauni milioni 35 kumsajili mshambuliaji wa Crystal Palace, Jean-Philippe Mateta, lakini Palace (Eagles) wanataka kifurushi cha pauni milioni 40 na watamruhusu Mfaransa huyo mwenye umri wa miaka 28 kuondoka ikiwa bei hiyo itafikiwa. (Athletic)

Juventus pia wanavutiwa na winga wa Liverpool, Mtaliano, Federico Chiesa, 28, na mshambuliaji wa Uholanzi Joshua Zirkzee, 24, ambaye yuko Manchester United . (Gazzetta dello Sport)

Mshambuliaji wa Everton na Guinea-Bissau Beto, 27, ni mojawapo ya chaguo la Juventus wanapotafuta kumsajili mshambuliaji wakati wa dirisha la uhamisho la majira ya baridi. (Gazzetta dello Sport)

Mshambuliaji wa Ufaransa Randal Kolo Muani, 27, yuko Tottenham kwa msimu mzima akitokea Paris St-Germain na ni chaguo jingine ambalo Juventus wanalitazama (Fabrizio Romano)

Kiungo wa kati wa Manchester United Bruno Fernandes anatarajiwa kusubiri hadi mwisho wa msimu kabla ya kuamua kuhusu mustakabali wake, huku mkataba wa sasa wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 ukiendelea hadi 2027 na akiwa na chaguo la kuongeza mwaka mmoja zaidi. (Mirror)

Atletico Madrid wanatarajiwa kufanya mazungumzo na Atalanta kuhusu kumsajili kiungo wa kati wa Brazil mwenye umri wa miaka 26 Ederson. (AS)

Everton wamekataa ofa kutoka Lazio kwa kiungo wa kati wa Uingereza, Tim Iroegbunam mwenye umri wa miaka 22. (Corriere dello Sport)

Beki wa Newcastle United , Mwingereza Jamal Lascelles, 32, ameambiwa anaweza kuondoka klabuni hapo ikiwa mkataba sahihi utapatikana. (Chronicle)

Wolves wamekataa ofa ya pauni milioni 6.9 kutoka Roma kwa ajili ya beki wa kushoto wa Norway mwenye umri wa miaka 23, David Moller Wolfe. (Sky Sports)

Meneja wa zamani wa Southampton na Rangers, Russell Martin ni miongoni mwa wanaotarajiwa kuchukua nafasi ya meneja wa Leicester City kufuatia kufukuzwa kwa Marti Cifuentes. (Football Insider)

Mchezaji wa zamani wa Leicester City, Gary Rowett na meneja wa Hearts, Derek McInnes pia wanafikiriwa na City. (Mail)

BBC

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
4m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
33m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’