Local,Transfer News,Simba

Simba yanasa winga mwingine kutoka Ivory Coast

Joel JJ By Joel JJ
β€’
27 Jan 2026
Simba yanasa winga mwingine kutoka Ivory Coast

Klabu ya Simba SC imeendelea kuimarisha kikosi chake baada ya kuthibitisha usajili wa kiungo mshambuliaji Anicet Oura, raia wa Ivory Coast, aliyekuwa akicheza soka la kulipwa nchini Finland.

Oura, mwenye umri wa miaka 26, amejiunga na Wekundu wa Msimbazi kama mchezaji huru kufuatia kumaliza mkataba wake na klabu ya IF Gnistan ya Finland, hatua inayompa Simba nyongeza muhimu kuelekea nusu ya pili ya msimu.

Nyota huyo anajulikana kwa uwezo wake wa kucheza nafasi zaidi ya moja uwanjani, akimudu winga wa kulia, winga wa kushoto pamoja na kiungo mshambuliaji namba 10, hali inayompa kocha Steve Barker chaguo pana katika kupanga kikosi chake.

Usajili wa Oura unaelezwa kuwa mapendekezo binafsi ya kocha Barker, ambaye aliwahi kufanya kazi na mchezaji huyo katika klabu ya Stellenbosch FC ya Afrika Kusini kabla Oura hajahamia Finland.

Katika msimu wa 2023/24 akiwa Stellenbosch, Oura alionyesha kiwango kizuri baada ya kufunga mabao nane katika mechi 35 alizocheza kwenye mashindano yote, akijijengea jina kama mchezaji mwenye mchango mkubwa kwenye eneo la mwisho la ushambuliaji.

Ujio wa Oura unatarajiwa kuongeza ubunifu, kasi na ushindani ndani ya kikosi cha Simba, hasa katika kipindi ambacho klabu hiyo inapambana kwenye mashindano ya ndani na kimataifa.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
3h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
7h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
10h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
13h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
13h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
13h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
15h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
19h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’