Local,Normal News,Yanga, Dodoma

Dodoma Jiji hoi mbele ya Yanga

Joel JJ By Joel JJ
β€’
27 Jan 2026
Dodoma Jiji hoi mbele ya Yanga

Yanga imerejea kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ya NBC baada ya kuichapa Dodoma Jiji mabao 3-1 katika mchezo uliopigwa uwanja wa KMC Complex.

Wananchi walilazimika kutokea nyuma kupata ushindi huo muhimu baada ya Dodoma Jiji kufunga bao la kutangulia kupitia William Edgar dakika ya 41.

Hata hivyo Yanga ilisawazisha bao hilo dakika ya 45 kupitia mkwaju wa penati uliowekwa kambani na Depu baada ya Frank Assink kufanyiwa madhambi ndani ya eneo la hatari.

Kipindi cha pili Yanga iliongeza kasi ya mashambulizi hasa baada kuingia kwa Duke Abuya, Allan Okello na Mohamed Damaro.

Wananchi waliongeza mabao mawili kupitia kwa Depu aliyefunga bao lake la tatu ndani ya mechi mbili kupitia mpira wa kichwa kabla ya Prince Dube kuongeza uongozi zaidi akitumia makosa ya safu ya ulinzi ya Dodoma Jiji ambao walipoteza mpira langoni kwao wakati wakijenga shambulizi kutokea nyuma.

Depu ameibuka nyota wa mchezo huo baada ya kufunga mabao mawili, pengine angeweza kuondoka na mpira kama angeongeza umakini.

Yanga imefikisha alama 22 na kurejea kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kucheza mechi nane.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
9h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
15h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
16h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
18h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
21h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’