International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi Januari 29 2026

Joel JJ By Joel JJ
β€’
29 Jan 2026
Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi Januari 29 2026

Juventus wanaongeza jitihada za kumsajili mshambuliaji wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 27, Randal Kolo Muani, ambaye yupo kwa mkopo Tottenham akitokea Paris St-Germain, na Spurs wanaweza kumchukua mshambuliaji wa Crystal Palace Jean-Philippe Mateta (28) kama mbadala endapo Kolo Muani ataondoka. (Mail)

Mshambuliaji wa Uholanzi Joshua Zirkzee pia ni chaguo lingine la Juventus, huku Manchester United sasa wakiwa tayari kumruhusu mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 kuondoka kwa mkopo. (Gazzetta dello Sport)

Manchester United pia wanatafakari mustakabali wa beki wa England Harry Maguire. Klabu hiyo haijafanya mazungumzo ya maana na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32, ambaye mkataba wake unaisha mwishoni mwa msimu huu. Tayari timu kadhaa kutoka Italia na Uturuki zimewasiliana na wakala wake. (Athletic)

Klabu za Ligi kuu ya Saudi Arabia zinapanga kumsajili mshambuliaji wa Paris St-Germain na Ufaransa Ousmane DembΓ©lΓ© (28) baada ya Kombe la Dunia la majira ya kiangazi. (Sky Sports)

PSG wameanza mazungumzo ya kuongeza mkataba wa kocha Luis Enrique, ambaye mkataba wake wa sasa na mabingwa wa Ligi ya Mabingwa unaisha mwaka 2027. (Le Parisien)

Kiungo mshambuliaji wa Uturuki Kenan Yildiz (20) amehusishwa na klabu kadhaa za ligi kuu England, lakini yuko karibu kuongeza mkataba wake ili kusalia Juventus. (Sky Sports Germany)

Atletico Madrid wanataka kumsajili kiungo wa Ujerumani Leon Goretzka, ambaye mkataba wake na Bayern Munich unaisha majira ya kiangazi, na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 anafikiria ofa hiyo. (Sky Sports Germany)

Klabu ya Serie A inayopambana kuepuka kushuka daraja Fiorentina imewasiliana na West Ham kuhusu kumsajili beki wa England Kyle Walker-Peters (28) na kiungo wa Ufaransa Soungoutou Magassa (22) kutoka kwa wapiga nyundo hao. (Gazzetta dello Sport, via Football Italia)

Bournemouth wako kwenye mazungumzo na Inter Milan kuhusu kumsajili winga Luis Henrique mwenye umri wa miaka 24. The Cherries wanapendekeza kumsajili kwa mkopo Mbrazil huyo kukiwa na kipengele cha kumnunua baadaye kwa takriban pauni milioni 18. (Talksport)

Jesse Lingard (33) yuko kwenye mazungumzo na klabu za England na Italia. Kiungo huyo wa zamani wa Manchester United, aliyechezea timu ya taifa ya England mara 32, ni mchezaji huru baada ya kuondoka FC Seoul mwezi Desemba. (Mail+)

River Plate wamekubaliana dili la kumsajili kiungo mshambuliaji wa Chelsea na Ecuador mwenye umri wa miaka 18, Kendry Paez, ambaye alitumia nusu ya kwanza ya msimu huu kucheza Strasbourg kwa mkopo. (Fabrizio Romano)

AC Milan wanatafuta beki na wanaweza kumnasa Radu Dragusin wa Tottenham. Beki huyo wa Romania mwenye umri wa miaka 23 pia anawindwa na Roma na Napoli. (Calciomercato)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
2h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
3h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
3h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
5h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
6h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
6h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
20h ago
READ MORE β†’