CAF yatembeza adhabu kwa Senegal, Morocco

Joel JJ By Joel JJ β€’ 29th January 2026


CAF yatembeza adhabu kwa Senegal, Morocco

Shirikisho la mpira wa miguu Afrika, CAF limeitoza Senegal faini ya jumla ya Sh1.55 Bilioni kufuatia ukiukwaji wa nidhamu katika fainali ya AFCON 2025 iliyopigwa Morocco.

Senegal imetozwa faini ya Sh756,300,000 milioni kwa kosa la utovu wa nidhamu kwa mashabiki, Sh756,300,000 milioni kwa utovu wa nidhamu kwa wachezaji na maafisa.

Pia imetozwa Sh37,815,000 kwa kosa la kupokea kadi tano za njano katika mchezo huo wa fainali. Mbali na hayo Kocha wa timu ya Taifa hilo na wachezaji wake wawili wamefungiwa mechi kadhaa na tutozwa faini kutokana na makossa mbalimbali waliyoyafanya.

Kocha wa Senegal Pape Thiaw amefungiwa mechi tano na kutozwa faini y Sh252 Milioni kwa kosa la kuhamasisha wachezaji wake kutoka uwanjani na kususia mchezo huo wa fainali 2025 waliocheza dhidi ya Morocco.

Licha ya kutishia kususia mchezo na baadhi ya wachezaji kurudi kwenye vyumba vya kubadilishia nguo, baada ya majadiliano ya muda ya wao kwa wao walikubaliana kurudi na kumalizia mchezo na baadae kuibuka mabingwa wa fainali hiyo kwa kuifunga Morocco bao 1-0 mchezo uliopigwa kwa dakika 120.

Wachezaji Iliman Ndiaye na Ismaila Sarr wamefungiwa kucheza mechi mbili kwa kosa la utovu wa nidhamu katika mchezo huo. Nyota hao walifanya kosa hilo kwa kuonyesha tabia isiyo ya kimichezo dhidi ya mwamuzi wa mechi hiyo wakionyesha kutoridhishwa na maamuzi aliyokuwa akiyatoa.

Aidha Morocco wametozwa faini jumla ya Sh805,612,000 kutokana na matukio yaliyojiri katika mchezo huo.

Mchezaji Achraf Hakimi amefungiwa mechi mbili kutokana na makosa ya utovu wa nidhamu aliyokutwa nayo na hatia. Wakati Ismael Saibari akifungiwa mechi tatu na faini ya zaidi ya Tsh 255,000,000.

Pia Morocco imeadhibiwa kwa makosa mengine yaliyotokana na vurugu za mashabiki na matumizi ya tochi yaliyopigwa marufuku na CAF


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.