Local,Transfer News,Coastal, Mazembe

Ulimwengu mbioni kutua Coastal Union

Joel JJ By Joel JJ
29 Jan 2026
Ulimwengu mbioni kutua Coastal Union

Klabu ya Coastal Union iko katika hatua za mwisho za kukamilisha usajili wa aliyekuwa straika wa TP Mazembe ya DR Congo, Thomas Ulimwengu baada ya mazungumzo ya pande mbili.

Ulimwengu amefungua milango na tayari kukitumikia kikosi cha Coastal Union kwa mkataba wa miezi sita hadi mwisho wa msimu huu.

 Nyota huyo aliyechezea timu za Soccer Akademia, Moro United, FC Vasby United, AFC Eskilstuna zote za Sweden, hakuwa na klabu yoyote ya ushindani tangu mara ya mwisho alipoachana na kikosi cha Fountain Gate, Julai 1, 2024.

Ulimwengu aliyecheza pia, TP Mazembe ya DR Congo, FK Sloboda Tuzla ya Bosnia and Herzegovina, Al-Hilal Omdurman ya Sudan na JS Saoura ya Algeria, ni pendekezo la Kocha wa Coastal Union, Mohamed Muya, anayetaka asajiliwe ili kuongeza nguvu.

Timu hiyo tayari imekamilisha usajili wa wachezaji watatu kipindi hiki cha dirisha dogo ambao ni Shiza Kichuya aliyecheza Simba na Namungo kisha msimu huu kuachana na JKT Tanzania, huku mwingine ni mshambuliaji, Abdulkarim Segeja aliyeondoka Tanzania Prisons. Nyota mwingine aliyejiunga na kikosi hicho ni mshambuliaji, James Msuva, ambaye hakuwa na timu pia.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
9h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
15h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
15h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
17h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
21h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →