International,Normal News,Local

Morocco wagonga mwamba malalamiko dhidi ya Ndala

Joel JJ By Joel JJ
β€’
30 Jan 2026
Morocco wagonga mwamba malalamiko dhidi ya Ndala

Mwamuzi wa mechi ya fainali AFCON 2025 kati ya Morocco dhidi ya Senegal Jean Jacques Ndala, hajapatikana na hatia baada ya uchunguzi kufanywa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF).

Baada ya uhakiki wa kina, CAF imethibitisha kuwa hakuna makosa yoyote ya uamuzi yaliyotokea katika mechi hiyo yanayomhusisha mwamuzi huyo kutoka DR Congo.

Morocco iliwasilisha malalamiko CAF wakimtuhumu mwamuzi huyo kuwa hakuwatendea haki katika mchezo huo pale aliposubiri kuchukua hatua baada ya wachezaji wa Senegal kugomea kuendelea na mchezo.

Baadae Senegal walirejea uwanjani na Ndala akaruhusu mkwaju wa penati ambapo Morocco walikosa na kulazimu mchezo kwenda muda wa nyongeza.

Senegal wakafunga bao la ushindi katika muda huo ambalo lilitosha kuwathibitisha kuwa mabingwa wa Afcon 2025.

Morocco walitarajia mwamuzi huyo angemaliza mchezo na wao kutwaa taji la Afcon pale Senegal walipogomea mchezo.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
7h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
10h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
14h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
16h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
17h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
19h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
22h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’