Local,Normal News,Yanga, Ahly

Kocha Yanga afunguka maandalizi kuikabili Al Ahly

Joel JJ By Joel JJ
β€’
30 Jan 2026
Kocha Yanga afunguka maandalizi kuikabili Al Ahly

Mkufunzi wa Yanga Pedro Goncalves amesema maandalizi kuelekea mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Al Ahly yamekamilika kikosi chake kikiwa tayari kukabiliana na mabingwa hao wa kihistoria Afrika.

Akizungumza katika mkutano na wanahabari kuelekea mchezo huo, Goncalves amesema wanakwenda kwenye mchezo huo kwa tahadhari kubwa huku dhamira yao ikiwa kuibuka na ushindi.

Goncalves amesema Al Ahly wana wachezaji wengi wenye ubora na uzoefu mkubwa, wanaweza kukuadhibu kwa kila kosa utakalofanya.

Amesema wamejiandaa kwenda kukabiliana nao huku wakiweka mkazo kwenye umakini wanapokuwa na mpira na hata bila ya mpira.

"Tunaamini tunaenda kukutana na timu ambayo ipo bora ikiwa na mpira na isipokuwa na mpira na sisi tunapaswa kuwa bora tukiwa na mpira na tusipokuwa na mpira"

"Tulicheza vyema kwenye mchezo wa kwanza lakini tulifanya makosa ambayo wapinzani wetu waliyatumia kutuadhibu, tumefanya maborehso muhimu naamini tutakuwa na mechi nzuri hapo kesho"

Akiwazungumzia Al Ahly, Goncalves amesema kukosekana kwa kiungo Emam Ashour ni pigo kwao lakini upande wa kikosi chake hilo sio jambo la kulifurahia kwa sababu Al Ahly wana wachezaji wengi wanaoweza kutumika nafasi ya Ashour.

"Wao kumkosa Emam Ashour ni pigo kwao lakini kwetu hatuwezi kusema ni faida moja kwa moj. Zizo huwa anacheza sana pale kwenye timu ya Taifa na hata alipoumia Emam yeye ndiye alicheza. Ni lazima tujiangalie sisi wenyewe kwanza, wale wana watu wenye uwezo mkubwa," aliongeza Goncalves

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
2h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
6h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
10h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
12h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
12h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
12h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
14h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
18h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’