Yanga yashusha winga dakika za jioooni

Joel JJ By Joel JJ β€’ 31st January 2026


Yanga yashusha winga dakika za jioooni

Dirisha la usajili limefungwa majira ya saa 5:59 usiku, Rais wa Yanga Injini Hersi Said akaamua dirisha hili lifungwe kinyonge.

'Usiku mnene' Yanga ikatambulisha usajili wa winga hatari raia wa Gambia, Buba Jammeh (24).

Hii ilikuwa sapraisi kwelikweli kwa Wananchi kwani ni usajili uliofanyika dakika za jioooni.

Buba ametua Yanga akitokea klabu ya Interclube ya Angola, akimudu kucheza nafasi zote za winga. Ni kama Yanga imeamua kuleta mbadala wa Ecua Celestin aliyetolewa kwa mkopo JS Kabylie kwani Buba nae anatumia mguu wa kushoto.

Ni wazi sasa usajili wake umemuondoa kiungo Moussa Balla Conte ambaye Yanga ilipokea ofa kadhaa kwa ajili yake ikiwemo klabu ya Raja CA.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.