International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Januari 31 2026

Joel JJ By Joel JJ
β€’
31 Jan 2026
Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Januari 31 2026

Curtis Jones wa Liverpool anavutia klabu ya Serie A, Inter Milan, huku Gabriel Jesus na Gabriel Martinelli wakitarajiwa kujiunga na La Liga.

Hata hivyo, Joshua Zirkzee anaonekana kwa sasa anaweza kusalia Ligi ya Primia. Inter Milan wako kwenye mazungumzo na Liverpool kuhusu uhamisho wa mkopo kwa kiungo Curtis Jones, 25, wakiwa na chaguo la kumnunua kiungo huyo wa kati wa Uingereza. (Fabrizio Romano)

Arsenal inaweza kuwauza washambuliaji wa Brazil Gabriel Jesus, 28, na Gabriel Martinelli, 24, kama sehemu ya mpango wa kumsajili mshambuliaji wa Atletico Madrid na Argentina Julian Alvarez, 25. (Teamtalk)

Arsenal pia wanakaribia kumuuza beki Oleksandr Zinchenko kwa Ajax. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ukraine mwenye umri wa miaka 29 alijiunga na Nottingham Forest kwa mkopo msimu uliopita wa joto lakini amecheza mechi nne pekee za Ligi Kuu. (Athletic - subscription required)

Nottingham Forest inafuatilia mpango wa kumsajili kipa wa Manchester City, Stefan Ortega, mwenye umri wa miaka 33, ambaye mkataba wake unaisha msimu huu wa joto. (Florian Plettenberg - Sky Germany)

Kiungo wa kati wa Everton Dwight McNeil, 26, ni chaguo jingine kwa Nottingham Forest, lakini juhuzi za Toffees kupata mbadala wa Mwingereza huyo zinaweza kufanya mpango huo kuwa mgumu. (Sky Sports)

Mshambuliaji wa Uholanzi Joshua Zirkzee, 24, anataka kubaki Manchester United kwa msimu wote uliosalia, baada ya kuhusishwa mara kwa mara na kurejea Italia huku Roma ikimtaka. (Sun)

Beki wa kati wa Argentina, Lautaro Rivero, wa River Plate, anafuatiliwa na Manchester City, Manchester United, Tottenham, Atletico Madrid, Juventus na Strasbourg. Kulingana na mkataba wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22, kwanza anafaa kutolewe pauni milioni 86 ili kuweza kuuzwa. (El Crack Deportivo - in Spanish)

Real Madrid wako tayari kumnunua kiungo wa kati wa Ufaransa Eduardo Camavinga, huku Arsenal na Liverpool zikiwa na hamu ya kumsajili mchezaji huyo wa miaka 23. (Fichajes - in Spanish)

Aston Villa wamepokea ofa ya mkopo kutoka Hoffenheim kwa ajili ya mshambuliaji wao wa Uskoti chini ya miaka 21 Rory Wilson, 20. (Sky Sports)

Wolves wana nia ya kumsajili mshambuliaji wa Scotland Che Adams, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 akiichezea timu ya Torino ya Italia tangu alipoondoka Southampton kwa uhamisho wa bure katika msimu wa joto wa 2024. (Talksport)

Karim Benzema anafikiria kurudi Ulaya au kutafuta klabu katika Ligi Kuu ya Soka baada ya majadiliano kuhusu mkataba mpya nchini Saudi Arabia kuwa mabaya. Mshambuliaji huyo wa zamani wa Real Madrid na Ufaransa mwenye umri wa miaka 38 atamaliza mkataba wake na Al-Ittihad mwezi Juni. (ESPN)

Manchester City wanafikiria kumrejesha kiungo wa kati wa Norway Sverre Nypan, 19, ambaye yuko kwa mkopo Middlesbrough, katika kikosi chao kwa msimu uliosalia. (Manchester Evening News)

Barcelona wanapanga dau la msimu wa joto kwa beki wa kati wa Manchester United na Argentina Lisandro Martinez, 28. (Fichajes - in Spanish)

BBC

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
2h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
6h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
10h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
12h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
12h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
12h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
14h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
18h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’