Local,Normal News,Simba, Esperance

Simba macho yote kwa Esperance

Joel JJ By Joel JJ
β€’
31 Jan 2026
Simba macho yote kwa Esperance

Klabu ya Simba SC inakabiliwa na mtihani mzito wa kufa au kupona itakapokutana na Esperance Tunis siku ya Jumapili katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, mechi inayotajwa kuwa ya maamuzi kwa hatma ya Wekundu wa Msimbazi katika kuisaka tiketi ya robo fainali ya michuano hiyo.

Mchezo huo unabeba uzito mkubwa siyo kwa kuwania pointi pekee, bali pia kwa kurejesha morali ya kikosi ambacho kimeanza mashindano hayo kwa matokeo yasiyoridhisha. Ndani ya Simba, kuna hali ya utayari na msisitizo mkubwa wa kuonyesha mshikamano na kupambana ili kubadili taswira ya timu kwenye hatua ya makundi.

Kocha Mkuu wa Simba Steve Barker amesema mchezo huo ni muhimu kwa timu nzima, akibainisha kuwa matokeo chanya yanaweza kuwa mwanzo wa kurekebisha makosa ya awali na kuijenga upya imani ya wachezaji pamoja na mashabiki.

"Ni kweli kwamba tumekutana na changamoto katika mechi zetu tatu za kwanza katika mashindano haya ya Ligi ya Mabingwa Afrika, lakini huo sio mwisho wa safari yetu, bado tuna nafasi ya kufanya kitu katika mechi ambazo zimesalia."

"Mechi dhidi ya Esperance ni muhimu sana kwetu, sio tu kwa sababu ya pointi, bali pia kwa morali ya kikosi chetu. Tunahitaji kuonyesha msimamo wetu kama timu. Tukipata matokeo chanya, inaweza kuwa mwanzo wa kurekebisha kilichotokea. Hii ni mechi ambayo tunahitaji sana, sapoti ya mashabiki wetu," alisema Barker

Msimamo wa Kundi D, Stade Malien ya Mali inaongoza kwa pointi saba, ikifuatiwa na Esperance Tunis yenye pointi tano, huku Petro Atletico ikishika nafasi ya tatu kwa pointi nne. Simba SC ipo mkiani mwa kundi hilo ikiwa bado haijapata pointi hata moja.

Hadi sasa, Simba imekuwa timu pekee katika kundi hilo kushindwa kuvuna pointi. Ilianza kwa kupoteza nyumbani kwa bao 1-0 dhidi ya Petro Atletico, ikafuata kipigo cha mabao 2-1 ugenini dhidi ya Stade Malien, kabla ya kupoteza tena kwa bao 1-0 dhidi ya Esperance.

Matokeo hayo yameifanya mechi ijayo dhidi ya Esperance kuwa ya lazima kushinda ili kufufua matumaini ya kusonga mbele. Simba inawahitaji mashabiki wake kwa wingi siku ya Jumapili kwani wao ni nguzo muhimu katika kuisukuma timu kupata matokeo chanya.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’