Mwamuzi wa kimataifa kutoka Afrika Kusini, Abongile Tom, ameteuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kusimamia mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya AS FAR ya MoroccoΒ na Young Africans SC ya Tanzania.
Mchezo huo ni wa raundi ya tano ya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) na unatarajiwa kuchezwa Jumamosi, Februari 7, 2026, nchini Morocco.





