Ambongile kuzihukumu AS FAR vs Yanga, CAFCL

Joel JJ By Joel JJ • 3rd February 2026


Ambongile kuzihukumu AS FAR vs Yanga, CAFCL

Mwamuzi wa kimataifa kutoka Afrika Kusini, Abongile Tom, ameteuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kusimamia mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya AS FAR ya Morocco na Young Africans SC ya Tanzania.

Mchezo huo ni wa raundi ya tano ya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) na unatarajiwa kuchezwa Jumamosi, Februari 7, 2026, nchini Morocco.

Abongile Tom ni miongoni mwa waamuzi waliobobea barani Afrika, akiwa na uzoefu mkubwa wa kusimamia michezo ya kimataifa yenye ushindani mkubwa. Uteuzi wake unaonesha dhamira ya shirikisho hilo kuhakikisha mchezo huo unaendeshwa kwa haki, nidhamu na weledi wa hali ya juu.

Mchezo kati ya AS FAR na Yanga unaelezwa kuwa wa maamuzi, kutokana na nafasi za timu hizo katika kundi. Matokeo ya mchezo huo yanaweza kuamua hatma ya kufuzu kwenda robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Kwa upande wa Yanga, ushindi katika mchezo huo unaweza kuwapa tiketi ya moja kwa moja ya kufuzu hatua ya robo fainali, huku sare ikipewa nafasi ya kuwaweka katika mazingira mazuri ya kufuzu, endapo watafanikiwa kushinda mchezo wao wa mwisho nyumbani dhidi ya JS Kabylie. Kipigo, hata hivyo, kitaifanya safari ya kufuzu kuwa ngumu zaidi.

Taarifa zinaeleza kuwa kikosi cha Yanga kinatarajiwa kuondoka jijini Dar es Salaam leo Jumanne kuelekea Morocco, kuanza maandalizi ya mwisho ya mchezo huo muhimu.

Mashabiki wa soka wanasubiri kwa hamu pambano hilo, linalotarajiwa kuwa miongoni mwa michezo mikubwa ya raundi hii ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.