Kocha Simba awapa tumaini mashabiki

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd February 2026


Kocha Simba awapa tumaini mashabiki

Kocha Mkuu wa Simba Steve Barker amewataka Wanasimba kuendelea kuwa wamoja huku akiahidi kikosi chake kupambana ili wamalize michuano ya ligi ya mabingwa kwa heshima na zaidi kufanya vyema katika mashindano mengine.

Juzi Barker alishuhudia kikosi chake kikipoteza uongozi wa mabao mawili kipindi cha kwanza na kulazimishwa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Esperance ya Tunisia matokeo ambayo yamefuta matumaini ya Simba kufuzu robo fainali.

Barker amesema walikuwa na mkakati mzuri walioukamilisha kwa usahihi katika kipindi cha kwanza lakini kukosekana kwa umakini na presha ya mchezo ikawagharimu kwenye lipindi cha pili na kuruhusu mabao mawili.

"Kufungwa mabao mawili na kushindwa kushinda kutoka kwenye nafasi tuliyokuwa nayo ni jambo linaloumiza, hasa kwa sababu wachezaji walifanya kazi kubwa sana kipindi cha kwanza"

"Tutaendelea kufanya kazi kwa bidii, kupambana kwa ajili ya beji ya Simba na kuhakikisha timu inaendelea kukua na kuwa bora zaidi, natambua hali ambayo mashabiki wetu wanajisikia, lakini hiki ni kipindi cha mpito na niwahakikishie kuna nyakati nzuri za furaha zinakuja ni suala la muda tu,” alisema Barker.

Kwa sasa Simba imesaliwa na mechi mbili katika hatua ya makundi kwa kucheza ugenini dhidi ya Petro Atletico huko Angola kabla ya kufunga pazia katika michuano hiyo kimataifa kwa kucheza dhidi ya vinara Stade Malien.

Mchezo dhidi ya Petro Atletico unatarajiwa kupigwa Jumamosi, Februari 07 huko Angola na kisha Simba kurejea Dar kumalizana na Stade Malien Februari 14


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.