Mapema leo, vyombo vya habari viliripoti taarifa inayohusu mashabiki wa Simba kufanya mkutano na waandishi wa Habari wakizungumzia mstabali mzima wa mwenendo wa timu yao.
Pamoja na mambo mengine waliyozungumza, wanachama hao walimtamtaka Mwekezaji wao Mohamed Dewji 'Mo' aondoke katika klabu yao ndani ya saa 72 ili watafute mwekezaji mwingine.
Wakati hayo yakijiri, uongozi wa Simba umetoa taarifa ya kutotambua Mkutano huo huku wakitangaza rasmi kuwachukulia hatua wahusika kwa kutumia nembo za wadhamini wa klabu hiyo bila ya ruhusa.
Taarifa iliyotolewa na Simba imebainisha kuwa, tayari wamelitaarifu jeshi la Polisi kuwachukulia hatua.

