Mzize bado kidogo Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th February 2026


Mzize bado kidogo Yanga

Mshambuliaji Clment Mzize ni miongoni mwa wachezaji waliosafiri na kikosi cha Yanga Morocco kuelekea mchezo dhidi ya AS FAR, raundi ya tano, kundi B ligi ya mabingwa barani Afrika.

Mzize ameendelea kuimarika baada ya kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu unaweza kusema ni suala la muda tu kwake kuonekana uwanjni.

Pengine mshambuliaji huyo ambaye aliongeza mkataba wa kuendelea kusalia Yanga kwenye dirisha la Julai licha ya timu nyingi kumuhitaji, anaweza kuwa tayari kurejea kwenye mchezo dhidi ya JS Kabylie utakaopigwa Februari 14

Mkufunzi wa Yanga Pedro Goncalves ameweka wazi kuwa hana mpango wa kumtumia Mzize katika mchezo dhidi ya AS FAR kwa kutambua umuhimu wa kumlinda na kuhakikisha harudi tena kwenye majeraha kama ilivyotokea huko nyuma

"Ni jambo jema kwetu kuona Clement (Mzize) anafanya mazoezi kikamilifu na timu, hatutakuwa na haraka kumtumia katika mechi hizi zenye presha kubwa kwani afya ya mchezaji ni kipaumbele kikubwa kuliko presha ya matokeo ya muda mfupi.," alisema

Jumamosi Yanga itakuwa ikisaka ushindi au angalau sare kwenye mchezo dhidi ya AS FAR ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kutinga hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.