International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Februari 07 2026

Joel JJ By Joel JJ
β€’
7 Feb 2026
Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Februari 07 2026

Ligi Kuu ya Saudi Arabia iko tayari kumuuza mshambuliaji wa Ureno Cristiano Ronaldo kwa ada ya pauni milioni 43. Hata hivyo, Manchester United hawana mpango wa kumrejesha nyota huyo mwenye umri wa miaka 41 kwa mara ya tatu. (The i paper)

Chelsea iko tayari kupambana na Tottenham Hotspur kuwania saini ya mshambuliaji wa Serbia Dusan Vlahovic, 26, ambaye mkataba wake na Juventus unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu. (Football Insider)

Mlinzi wa zamani wa Hispania Sergio Ramos, 39, ambaye yuko huru hana klabu, anataka kujiunga na Marseille baada ya klabu yake ya tangu utotoni Sevilla kugoma kumsajili tena. (Radio Marca)

Fulham wameanza tena mazungumzo na PSV Eindhoven na wana matumaini ya kukamilisha uhamisho wa mshambuliaji wa Marekani Ricardo Pepi, 23, dirisha la kiangazi. (Teamtalk)

Chelsea iko tayari kumruhusu mlinzi wao Mfaransa Benoit Badiashile, 24, kuondoka msimu wa kiangazi, huku AC Milan, Juventus na Marseille zikifuatilia kwa karibu suala lake. (Caughtoffside)

Manchester City wanapanga kumsajili kiungo wa Nottingham Forest na timu ya taifa ya England Elliot Anderson, 23, beki wa kulia wa Brentford na timu ya vijana ya Italia Michael Kayode, 21, pamoja na beki wa kulia wa Feyenoord na timu ya vijana ya Uholanzi Givairo Read, 19. Hatua hii inachangiwa na imani kuwa kocha Pep Guardiola atasalia klabuni kwa angalau msimu mmoja zaidi. (The i paper)

Arsenal watapambana na AC Milan kuwania saini ya kiungo wa Ujerumani Leon Goretzka, 31, baada ya Bayern Munich kuthibitisha kuwa ataondoka klabuni humo msimu wa kiangazi kwa uhamisho wa bure. (Calciomercato)

Wakala wa kiungo wa Newcastle United na timu ya taifa ya Italia Sandro Tonali, ambaye anasakwa na Arsenal, amesema uamuzi kuhusu mustakabali wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 utajulikana mwishoni mwa msimu. (Tuttosport)

Newcastle United wanamfuatilia kiungo wa Liverpool Curtis Jones, 25, kama mbadala wa Tonali endapo ataondoka, lakini Tottenham Hotspur na Aston Villa pia wanaonyesha nia ya kumsajili mchezaji huyo wa England. (Teamtalk)

Napoli bado wanamuwania mshambuliaji wa England Raheem Sterling, 31, ambaye kwa sasa hana klabu, lakini watamsajili tu endapo atakubali kupunguza kwa kiasi kikubwa mshahara wake wa euro milioni 19 kwa mwaka (pauni milioni 16.4). (Calciomercato)

Liverpool na Manchester United ni miongoni mwa klabu za hivi karibuni za Ligi Kuu England kuonyesha nia ya kumsajili winga wa RB Leipzig na Ivory Coast Yan Diomande, 19. (Football Insider)

Chelsea wameelekeza macho yao kwa mshambuliaji wa Porto Samu Aghehowa, 21, lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa Tottenham Hotspur na Newcastle United wanaomtaka pia mshambuliaji huyo wa Uhispania. (Teamtalk)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
48m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’