Stade Malien ilivyozima Esperance, Simba kundi D

Joel JJ By Joel JJ • 9th February 2026


Stade Malien ilivyozima Esperance, Simba kundi D

Stade Malien imekuwa timu ya kwanza kukata tiketi ya robo fainali michuano ya ligi ya mabingwa kutoka kundi D baada ya kuichapa Esprance bao 1-0 hapo jana.

Baada ya ushindi huo, Stade Malien walifikisha alama 11 na kujihakikisha kuongoza kundi D, kwani hakuna timu nyingine inaweza kufikisha alama hizo katika kundi.

Esperance na Petro Atletico kila moja ina alama sita mechi ya mwisho baina yao itaamua timu ya kutinga robo fainali sambamba na Stade Malien.

Kilichofanywa na Stade Malien hakikutarajiwa kwani baada ya droo ya makundi ni Simba na Esperance zilizokuwa zikipewa nafasi ya kuvuka katika kundi hilo.

Katika ranking za CAF Esperance wako nafasi ya tatu huku Simba wakiwa nafasi ya tano Stade Malien hawamo hata kwenye 20 bora lakini msimu huu wamewashangaza wengi, ikiwa timu pekee ambayo haijapoteza mchezo kundi D.

Unaweza kusema wamenufaika kwa kuporomoka kiwango kwa klabu za Simba na Esperance lakini pia wana kikosi bora.

Malien wanaweza kufanya vyema  hatua inayofuata na pengine hata kufika nusu fainali kama wataendeleza kiwango chao cha sasa.

Mechi ya mwisho kundi D watasafiri Dar es salaam kuumana na Simba katika mchezo utakaopigwa Februari 14 katika uwanja wa Benjamin Mkapa.

Kwa Simba huu utakuwa mchezo wa kisasi baada ya kupoteza mchezo wa kwanza timu hizo zilipokutana Mali ingawa matokeo yake hayatakuwa na athari yoyote kwenye msimamo wa kundi.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.