Local,Normal News,Yanga, Ahly, Kabylie, FAR

Yanga yapania kufuzu robo fainali mbele ya JS Kabylie

Joel JJ By Joel JJ
β€’
9 Feb 2026
Yanga yapania kufuzu robo fainali mbele ya JS Kabylie

Yanga inatarajiwa kurejea leo kutoka Morocco baada ya mchezo wa raundi ya tano ligi ya mabingwa kundi B wakikubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa AS FAR.

Baada ya kurejea, hakutakuwa na muda wa kupoteza kwani vijana wa kocha Pedro Goncalves wanapaswa kuanza maandalizi ya mchezo wa maamuzi dhidi ya JS Kabylie ambao utapigwa Jumapili, Februari 15.

Kimahesabu Yanga bado ina nafasi ya kufuzu robo fainali, pamoja na kuwa watategemea matokeo ya mchezo kati ya Al Ahly dhidi ya AS FAR.

Ushindi kwa Al Ahly utafungua milango kwa Yanga kufuzu lakini Wananchi watahitaji kushinda kuanzia mabao mawili au zaidi ili kunufaika.

Kazi kubwa ambayo kocha Goncalves atahitaji kuifanya katika siku chache zilizobaki ni kuimarisha safu yake ya ushambuliaji hasa kwenye matumizi ya nafasi.

Katika mchezo dhidi ya AS FAR, kulikuwa na uwezekano wa Yanga kufunga zaidi ya mabao mawili kama washambuliaji wangetumia nafasi kwa usahihi.

Katika mchezo ujao hakutakuwa na lugha nyingine kama Yanga itakosa ushindi, hata kama AS FAR watapoteza dhidi ya Al Ahly watafuzu.

JS Kabylie hawatakuwa na cha kupoteza katika mchezo huo kwani tayari wamepoteza matumaini ya kusonga mbele hivyo hawatarajiwi kuja na mpango wa 'kupaki basi'.

Unatarajiwa kuwa mchezo wa wazi ambao pengine nafasi nyingi zitatengenezwa kwa kila upande.

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
4m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
33m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’