Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' Miguel Gamondi amesaini mkataba wa miaka miwili kuendelea kukinoa kikosi cha Taifa Stars.
Gamondi ambaye alipewa majukumu ya muda kuiongoza Stars kwenye michuano ya Afcon 2025, amepewa mkataba wa muda mrefu baada ya kufanya vyema akiingoza Stars kucheza hatua ya 16 bora kwa mara ya kwanza.
Atahudumu kwenye nafasi hiyo hadi mwaka 2028 akitarajiwa kuiongoza Stars kwenye michuano ya Afcon 2027 Tanzania ikiwa nchi mwenyeji pamoja na Kenya n Uganda.





