Bodi ya ligi (TPLB) imetangaza mchezo wa namba 154 ligi kuu ya NBC kati ya Yanga dhidi ya Simba utapigwa March 1, 2026 katika uwanja wa New Amaan Complex.
Mchezo huo wa pili kuzikutanisha Simba na Yanga msimu huu baada ya kukutana kwenye Ngao ya Jamii, utapigwa saa 2:15 usiku.
Yanga ni wenyeji wa mchezo huo, TPLB ikiridhia ombi lao la kuchezwa Zanzibar.





