Local,Normal News,Simba

BMT yamaliza utata Katiba ya Simba

Joel JJ By Joel JJ
β€’
18 Feb 2026
BMT yamaliza utata Katiba ya Simba

Serikali kupitia Baraza la Michezo la Taifa (BMT) imeidhinisha rasmi marekebisho ya katiba ya Simba Sports Club baada ya kukamilika kwa mchakato wa kisheria chini ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Michezo.

Uidhinishaji huo unaipa Simba mwanga wa kuanza utekelezaji wa katiba mpya inayolenga kuimarisha utawala bora, kuongeza uwajibikaji na kuweka mazingira rafiki kwa uwekezaji katika klabu hiyo kongwe nchini.

Kwa mujibu wa marekebisho hayo, imewekwa bayana kuwa Simba Sports Club Company Limited ndiyo chombo kitakachosimamia masuala ya kibiashara na kiutendaji ya klabu. Hatua hiyo inalenga kutenganisha majukumu ya kiutawala na yale ya kibiashara kwa lengo la kuongeza ufanisi na ushindani katika soka la kisasa.

Aidha, umiliki wa hisa utaendelea kubaki chini ya Baraza la Wadhamini kwa niaba ya wanachama wa klabu, hatua inayolenga kulinda misingi ya umiliki wa wanachama na kuhakikisha maslahi yao yanabaki salama. Katiba hiyo pia imeainisha kuwa Baraza la Wadhamini litakuwa na wajumbe kati ya watano hadi saba, huku Mkutano Mkuu ukiendelea kuwa chombo chenye mamlaka ya mwisho ya maamuzi.

Akizungumza kuhusu uidhinishaji huo, Msajili wa Vyama vya Michezo, Abel Mathias Ngilungwa, amesema marekebisho hayo yamezingatia taratibu zote za kisheria na hayana athari kwa usalama wala hayachochei migogoro miongoni mwa wanachama.

Amesema lengo la mabadiliko hayo ni kuimarisha misingi ya utawala bora, kulinda umiliki wa klabu na kuweka mazingira yatakayovutia uwekezaji zaidi, hatua inayotarajiwa kusaidia maendeleo ya Simba ndani na nje ya uwanja.

Wanachama na mashabiki wa Simba wametakiwa kuheshimu uamuzi huo na kushirikiana katika utekelezaji wa katiba mpya kwa manufaa ya klabu. Wadau wa michezo wanaamini kuwa mageuzi hayo yanaweza kuwa chachu ya mafanikio mapya kwa Simba katika mashindano ya ndani na kimataifa.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
6h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
10h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
16h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
16h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
18h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
22h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’