Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wilfred Kidao, ametajwa kuwa mjumbe wa Bodi ya Usimamizi ya TRA United Sports Club.
Bodi hiyo imeznduliwa rasmi jana na Kamishna Mkuu wa TRA, Yusuph Juma Mwenda.
Bodi hiyo itaongozwa na mwenyekiti Edmund Kawamala, akishirikiana na wajumbe wengine nane kutoka sekta mbalimbali, wakiwemo viongozi wa Taasisi za Sekta Binafsi na watumishi wa TRA.
Lengo kuu la Bodi hiyo ni kuisimamia kikamilifu TRA United, kuifanya kuwa timu tishio ndani na nje ya nchi, huku ikitumia michezo kama njia ya kuelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa kulipa kodi kwa hiari.
Kamishna Mwenda amesisitiza kuwa timu hiyo imeanzishwa si kwa ajili ya burudani pekee, bali pia kufungamanisha wajibu wa TRA na wananchi.
โTumetengeneza timu hii kufundisha wananchi umuhimu wa kulipa kodi na kuhakikisha inakuwa mfano wa nidhamu na utendaji mzuri,โ amesema Mwenda.