Local, Yanga

Kamwe afunguka Yanga kucheza chini ya kiwango

Joel JJ By Joel JJ
β€’
19 Feb 2026
Kamwe afunguka Yanga kucheza chini ya kiwango

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe amesema ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Cosmopolitan katika mchezo wa hatua ya 32 bora kombe la CRDB, ni matokeo muhimu kwao kwani wamekata tiketi ya kufuzu hatua ya 32 bora.

Kamwe amesema lengo lao kwenye mchezo huo ilikuwa ushindi na kusonga mbele bila ya kujali idadi ya mabao waliyofunga.

Kamwe ametoa kauli hiyo kuwajibu wale waliobeza ushindi huo wakiamini Yanga ilipaswa kufunga mabao mengi dhidi ya timu hiyo inayoshiriki ligi ya Championship.

Msemaji huyo wa mabingwa wa nchi amesema Yanga imetoka kucheza mechi ngumu za ligi ya mabingwa na pia wakikabiliwa na mfululizo wa mechi hivyo ilikuwa muhimu kwa benchi la ufundi na wachezaji kuchukua tahadhari.

"Nimeona maoni ya watu wengi walitaka tufunge mabao mengi, huo sio mpira wa miguu. Tumetoka kwenye mechi ngumu Jumapili, tumerudi Jumatatu kwa maana yake tumefanya mazoezi siku moja tu na kwa asilimia kubwa wamecheza wale wale waliotumika Jumapili."

"Hizi ni mechi za kurefresh, cha muhimu unapata matokeo unakwenda kwenye hatua inayofuata. ‎Tuna mechi nyingine, Jumapili dhidi ya Namungo kule Ruangwa lakini pia tutakuwa na mechi tarehe 25 dhidi ya JKT hapa KMC Complex."

"Kwahiyo ni lazima wachezaji wetu wacheze kwa umakini mkubwa ili pia kujiepusha na majeraha na ndio maana wamecheza kwa tempo ya kawaida," alisema Kamwe

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
2h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
3h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
4h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
5h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
20h ago
READ MORE β†’