Local, Simba

Beki Simba nje hadi mwisho wa msimu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
19 Feb 2026
Beki Simba nje hadi mwisho wa msimu

Inaelezwa beki wa kati wa Simba Abdulrazack Hamza atakuwa nje kwa muda mrefu ambapo nyota huyo huenda akawa ameumaliza msimu.

Hamza alipata jeraha katika mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga Septemba 16 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Stadium, ambapo Simba ilipoteza kwa bao 1-0. Tangu wakati huo, beki huyo hajarejea uwanjani.

Baada ya tathmini ya kitabibu, mchezaji huyo alipelekwa nchini Morocco kwa matibabu zaidi katika Kliniki ya Zerktouni ambako alifanyiwa upasuaji Desemba Mosi mwaka jana. Awali kulikuwa na matumaini kuwa angeweza kurejea mapema katika mzunguko wa pili wa ligi, lakini hali imekuwa tofauti.

Chanzo cha ndani ya klabu kimebainisha kuwa ingawa maendeleo yake ni mazuri, madaktari wamependekeza apate muda mrefu zaidi wa mapumziko na uangalizi maalum ili kuhakikisha anapona kikamilifu kabla ya kurejea dimbani.

“Kwa sasa anaendelea vizuri, lakini taratibu za kitabibu zinaonyesha hatarudi uwanjani hadi msimu uishe. Jeraha lilikuwa kubwa kuliko ilivyodhaniwa mwanzo,” kilieleza chanzo hicho.

Msimu huu Simba imekabiliwa na changamoto katika safu yake ya ulinzi kwani wakati wakimkosa Hamza, pia Wekundu hao wa Msimbazi wanamkosa Wilson Nangu aliyefanyiwa upasuaji wa kifundo cha mguu Afrika Kusini jana.

Nangu aliumia kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Esperance uliopigwa dimba la Mkapa na kumalizika kwa sare ya mabao 2-2.

Kwa sasa eneo hilo linawategemea zaidi nahodha msaidizi Rushine de Reuck na Ismail Toure aliyesajiliwa kwenye dirisha dogo.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
2h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
3h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
4h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
5h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
20h ago
READ MORE β†’