Local,Normal News,Simba, Prisons

Barker aitangazia hatari Tanzania Prisons

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Feb 2026
Barker aitangazia hatari Tanzania Prisons

Kocha Mkuu wa Simba Steve Barker amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa ligi kuu dhidi ya Tanzania Prisons ambao utapigwa kesho Jumapili katika uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma.

Barker amesema wamekuwa na wakati mzuri wa kujiandaa na mchezo huo wakitua mkoani Dodoma jana ambapo leo watakuwa na nafasi ya kukamilisha maandalizi yao.

Kocha huyo raia wa Afrika Kusini amesema anatambua hakuna mechi nyepesi kwenye ligi kuu ya NBC hivyo hawatawadharau wapinzani wao.

"Sisi tumejiandaa vyema kwa ajili ya mchezo dhidi ya Tanzania Prisons hapo kesho. Maandalizi yetu yanakwenda vyema na kwa takribani miezi miwili niliyokuwa hapa tumekuwa na maandalizi ya kimbinu na uchezaji wetu"

"Jana baada ya safari ndefu tulifanya mazoezi ytu ya kwanza hapa na leo tutakamilisha maandalizi yetu."

"Natambua hakuna mechi nyepesi, tunafahamu wapinzani watatupa upinzani wa kutosha licha ya kuwa hawako kwenye nafasi nzuri katika msimamo wa ligi. Tumefanya maandalizi mazuri ya kimbinu na kiakili ili wachezaji wangu waende kufanya vizuri kwenye mchezo huu," alisema Barker

Wekundu hao wa Msimbazi wataikabili Tanzania Prisons kesho Jumapili katika mchezo utakaopigwa saa 3 usiku.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
2h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
6h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
10h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
12h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
12h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
12h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
14h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
18h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’