Mshambuliaji wa Kimataifa wa DR Congo Fiston Mayele ambaye anaitumikia klabu ya Pyramids inayoshiriki ligi kuu ya Misri, ameweka rekodi mpya katika klabu hiyo.
Baada ya kukaa kwa takribani miezi minne bila kufunga bao, jana Mayele aliifungia Pyramids katika ushindi wa mabao 3-1 dhidi y Ghazi El Mahalla.
Hilo lilikuwa bao la 50 kwa Mayele tangu ajiunge na timu hiyo akitokea klabu ya Yanga ya Tanzania misimu miwili iliyopita.
Mayele sasa ndiye mshambuliaji aliyefunga mabao mengi zaidi katika historia ya Pyramids.
Amefunga zaidi ya mabao 100 tangu alipokuwa Yanga na sasa Pyramids.



