Local,Normal News,Simba, Dodoma

Wachezaji Simba wampa matumaini Barker licha ya sare dhidi ya Dodoma Jiji

Joel JJ By Joel JJ
β€’
26 Feb 2026
Wachezaji Simba wampa matumaini Barker licha ya sare dhidi ya Dodoma Jiji

Kocha Mkuu wa Simba Steve Barker amewapongeza wachezaji wa timu hiyo kwa kiwango walichoonyesha kwenye mchezo wa ligi kuu dhidi ya Dodoma Jiji jana ambao ulimalizika kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana.

Akizungumza baada ya mchezo huo uliopigwa uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma, Barker alisema wachezaji wake walicheza kwa kujitoa sana lakini kilichokosekana ni alama tatu tu.

"Nawapongeza wachezaji wangu kwa kile walichoonyesha leo (jana). Tumecheza mechi ngumu sana lakini nimeridhishwa na jinsi timu ilivyocheza."

"Tumecheza kwa kujitolea sana, nafikiri kuna vitu vichache vya kuongeza ili tuwe bora zaidi. Kama tutaendelea kucheza hivi, tutashinda mechi nyingi," alisema Barker

Akizungumzia mchezo unaofuata dhidi ya Yanga ambao utapigwa Jumapili March 1 uwanja wa New Amaan Complex visiwani Zanzibar, Barker alisema wanakwenda kufanya maandalizi sahihi kuelekea mchezo huo wa dabi ya Kariakoo.

Barker amesema kikosi chake kitaelekea Zanzibar mapema ili kwenda kukamilisha maandalizi hayo akileta kushinda mchezo huo.

"Mechi dhidi ya Yanga tutajiandaa kama tunavyojiandaa kwenye mechi nyingine, tutahakikisha tunajiandaa vizuri. Tutafanya recovery na kisha kuelekea Zanzibar mapema iwezekanavyo."

"Hii ni dabi kubwa hivyo tutahakikisha tunajiandaa ili tuweze kupata alama tatu," alisema Barker

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
9h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
15h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
16h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
18h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
21h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’