Azam Fc imeendeleza ubabe kwenye ligi kuu ya NBC baada ya kuichapa Mtibwa Sugar mabao 3-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Azam Complex Jumatano usiku.
Mshambuliaji Mcongomani Jacques Ngita alikuwa shujaa wa Azam Fc katika mchezo huo akifunga mabao mawili.
Feisal Salum 'Fei Toto' ndiye aliyefungua milango ya Mtibwa Sugar kwa goli la mapema kabla yha Ngita kuongeza mengine mawili.
Ni kipigo cha tatu mfululizo kwa Mtibwa Sugar ambao mchezo uliopita pia walifungwa mabao 3-1 na Singida BS.
Azam Fc wamechupa hadi nafasi ya tano kwenye msimmo wa ligi wakifikisha alama 22, alama moja nyuma ya Simba yenye alama 23 nfasi ya tatu.
Simba ililazimishwa suluhu ya bila kufungana dhidi ya Dodoma Jiji mchezo uliopigwa mapema uwanja wa Jamhuri.
JKT Tanzania iliyokubaki kipigo cha mabao 5-0 kutoka kwa Yanga inaendele kushikilia nafasi ya pili ikiwa na alama 28 sawa na Yanga ambayo ulishindi wao dhidi ya JKT Tanzania umewapeleka kileleni mwa msimamo wa ligi.
