Klabu ya TRA United iliyokuwa na makazi yake mkoani Tabora sasa imehamia rasmi mkoani Arusha ambako itacheza mechi zake za nyumbani za ligi zinazofuata katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid.
Timu hiyo imepokelewa rasmi na mkuu wa mkoa wa Arusha CPA Amos Makalla mapema leo na kuanza maisha mapya mkoani humo.
Ikumbukwe kuwa TRA United inakuwa timu ya pili ya ligi kuu kuhamia mkoani humo ikitanguliwa na Fountain Gate FC iliyohama mkoani Manyara na kutua jijini Arusha.
Sasa wakazi wa Arusha watakuwa na uhakika wa kushuhudia mechi za ligi kuu hasa vigogo wa soka nchini klabu za Simba na Yanga ambazo zina mashabiki kila kona ya Tanzania.
