Ligi Kuu ya NBC imeendelea leo ambapo mechi mbili zilipigwa mkoani Singida na Mwanza.
Wenyeji Singida Black Stars walitumia vyema uwanja wa nyumbani wakiichapa Coastal Union bao 1-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Airtel.
Bao pekee la ushindi kwa Singida BS lilifungwa na mshambuliaji Joseph Guede.






