Local,Normal News,Azam, Singida, Coastal, Pamba

Azam Fc chupuchupu Mwanza, Singida BS yatamba nyumbani

Joel JJ By Joel JJ
β€’
2 Mar 2026
Azam Fc chupuchupu Mwanza, Singida BS yatamba nyumbani

Ligi Kuu ya NBC imeendelea leo ambapo mechi mbili zilipigwa mkoani Singida na Mwanza.

Wenyeji Singida Black Stars walitumia vyema uwanja wa nyumbani wakiichapa Coastal Union bao 1-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Airtel.

Bao pekee la ushindi kwa Singida BS lilifungwa na mshambuliaji Joseph Guede.

Mkoani Mwanza Azam Fc imenusurika na kichapo mbele ya Pamba Jiji wakilazimisha sare ya mabao 2-2.

Pamba Jiji ilijipatia bao la kwanza dakika ya 45 kupitia kwa kiungo wa Azam, Himid Mao, aliyejifunga (OG) wakati akijaribu kuokoa shambulizi. Mapema kipindi cha pili, dakika ya 48, John Ben Nakibinge aliipatia Pamba bao la pili na kuifanya Azam ionekane kuelekea kupoteza mchezo huo.

Hata hivyo, mabadiliko ya mbinu ya kocha Florent Ibenge yalizaa matunda haraka. Ndani ya dakika tatu za maajabu, Azam walirudi mchezoni: Dakika ya 56: Jean Jaques Ngita aliifungia Azam bao la kwanza. Dakika ya 59: Kiungo fundi, Feisal Salum 'Fei Toto', alisawazisha kwa mkwaju wa penalti.

Hata hivyo Feisal hakumaliza mchezo huo akitolewa kwa kadi nyekundu baada ya kumfanyia madhambi mlinzi wa Pamba Jiji Abdulmajid Mangalu.

Feisal anatarajiwa kukosa mechi mbili lakini ni wazi atauwahi mchezo wa dabi dhidi ya Yanga utakaopigwa March 15

Matokeo haya yameleta mabadiliko kidogo kwenye msimamo wa Ligi Kuu, Pamba Jiji FC imefikisha pointi 24 baada ya kucheza mechi 15, wakisalia katika nafasi ya nne.

Azam FC: Wamefikisha pointi 23 katika michezo 11, wakishika nafasi ya tano huku wakiwa na faida ya michezo minne mkononi dhidi ya Pamba.

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
4m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
34m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’