Al Ittihad imelipa mabilioni kuwanasa Aziz Ki, Lorch

Joel JJ By Joel JJ • 3rd March 2026


Al Ittihad imelipa mabilioni kuwanasa Aziz Ki, Lorch

Klabu kongwe ya Libya, Al-Ittihad Club, imekamilisha rasmi malipo ya ada za uhamisho kwa mabingwa wa Morocco, Wydad Athletic Club, kwa ajili ya kuwasajili nyota wawili waliokuwa wakikitumikia kikosi hicho.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, jumla ya dola za Marekani milioni 1.4 (takribani Sh3.9 bilioni) zimelipwa kukamilisha dili hilo. Kati ya fedha hizo, dola 800,000 (Sh2.04 bilioni) zimelipwa kwa ajili ya kiungo mshambuliaji Stephane Aziz Ki, huku dola 600,000 (Sh1.53 bilioni) zikihusu uhamisho wa winga wa Afrika Kusini, Thembinkosi Lorch.

Kukamilika kwa miamala hiyo kunahitimisha rasmi mchakato wa usajili wa wachezaji hao ambao tayari wameanza kuitumikia Al-Ittihad katika msimu wa 2025/26.

Aziz Ki, ambaye aliwahi kung’ara katika Ligi Kuu Tanzania Bara kabla ya kujiunga na Wydad, amekabidhiwa jezi namba 22, huku Lorch akikabidhiwa jezi namba 11 katika kikosi hicho cha Tripoli.

Usajili wa nyota hao unaonyesha dhamira ya Al-Ittihad kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu mpya, huku Wydad wakikamilisha mchakato wa uhamisho kwa mafanikio ya kifedha.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.