Baada ya mchezo dhidi ya Simba uliopigwa visiwani Zanzibar na kumalizika kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana, mabingwa watetezi wa ligi kuu ya NBC Yanga wanaeleka mkoani Singida ambako wanakabiliwa na mechi nyingine ngumu.
March 05 Yanga itakuwa dimba la Airtel huko Singida kuikabili Singida Black Stars katika mchezo mwingine unaotarajiwa kuwa na upinzani mkali.





