Local,Normal News,Simba

Bado tuko kwenye mbio za ubingwa - Magori

Joel JJ By Joel JJ
β€’
3 Mar 2026
Bado tuko kwenye mbio za ubingwa - Magori

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi klabu ya Simba Crescentus Magori amesema dhamira ya Wekundu hao wa Msimbazi msimu huu ni kuwania ubingwa wa ligi kuu.

Magori amewataka mashabiki na wanachama wa timu hiyo kuunga mkono uongozi wao katika mapambano ya kurejesha heshima yao kwenye soka la ndani.

Akizungumza baada ya mchezo dhidi ya Yanga uliopigwa uwanja wa New Amaan Complex visiwani Zanzibar juzi na kumalizika kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana, Magori aliwapongeza wachezaji wa Simba kwa kuonyesha kiwango kizuri katika mchezo huo ambao anaamini walistahili kupata ushindi.

"Sisi tuko imara na tunapigania ubingwa, Wanasimba wote tuache fitna na ugomvi hii timu itakuwa nzuri zaidi ya hapa ilipo."

"Mechi zetu zinakuwa ngumu sana lakini ni mechi za ukweli, mechi za halali na hazina maigizo. Tutaendelea kucheza hivyo," alisema Magori.

Suluhu dhidi ya Yanga imeendelea kuiweka Simba katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi wakifikisha alama 24.

Simba tayari imerejea jijini Dar kujiandaa na mechi zinazofuata ambapo March 08 watacheza mechi ya hatua ya 32 bora kombe la CRDB dhidi ya B19 itakayopigwa uwanja wa Isamuhyo.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
9h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
15h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
15h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
17h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
21h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’