Yanga kuikabili Singida BS bila Job, Azam Fc bila Fei Toto mikononi mwa Tanzania Prisons

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th March 2026


Yanga kuikabili Singida BS bila Job, Azam Fc bila Fei Toto mikononi mwa Tanzania Prisons

Mikiki mikiki ya ligi kuu ya NBC inaendelea leo ambapo mechi mbili zinatarajiwa kupigwa mkoani Singida na Mbeya.

Mabingwa watetezi wa ligi hiyo Yanga wako Singida majira ya saa 10 jioni wakitarajiwa kushuka uwanja wa Airtel kuwakabili wenyeji wao Singida Black Stars katika mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkali.

Katika mchezo huo Yanga itamkosa nahodha wake msaidizi beki Dickson Job ambaye alipata majeraha ya goti kwenye mchezo uliopita dhidi ya Simba.

Mkufunzi wa Yanga Pedro Goncalves pia jana alithibitisha kukosekana kwa Pacome Zouazoua na Edmund John wote wakiwa wanakabiliwa na changamoto za majeraha.

Mchezo mwingine unatarajiwa kupigwa mkoani Mbeya ambapo wenyeji Tanzania Prisons wataikaribisha Azam Fc.

Prisons wametoka kupoteza mchezo uliopita dhidi ya Simba wakati Azam Fc walilamisishwa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Pamba Jiji katika mchezo uliopita.

Azam Fc leo watamkosa kiungo wao fundi Feisal Salum ambaye anatumikia adhabu ya kukosa mechi mbili baada ya kadi nyekundu aliyopewa kwenye mchezo dhidi ya Pamba Jiji.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.