Local,Normal News,Azam, Prisons

Ibenge alia na ubovu wa uwanja Sokoine

Joel JJ By Joel JJ
β€’
6 Mar 2026
Ibenge alia na ubovu wa uwanja Sokoine

Jana Azam Fc ilishindwa kuondoka na alama zote tatu mkoani Mbeya baada ya kulazimishwa suluhu ya bila kufungana dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo wa ligi kuu ya NBC.

Wakati Kocha wa Tanzania Prisons Shadrack Nsajigwa akifurahia alama hiyo moja, Florent Ibenge wa Azam Fc amelalamika timu yake kukosa matokeo kwa sababu ya ubovu wa uwanja wa Sokoine.

"Ni ngumu kupata ushindi katika mazingira kama haya. Huu sio uwanja wa kucheza mpira wa miguu. Unapocheza katika uwanja kama huu hakuna ufundi, wachezaji wanalazimika kupiga tu mpira".

"Sio kama tunalalamika, tunazungumza uhalisi na jambo muhimu kwetu tumeweza kuondoka na alama moja kwa hiyo tunakwenda kujiandaa na mechi nyingine zinazofuata," alisema Ibenge.

Huo ulikuwa mchezo wa pili mfululizo Azam Fc inakosa ushindi ugenini baada ya kulazimishwa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Pamba Jiji katika mchezo uliopita.

Wauza Ice cream hao wamepanda nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi wakifikisha alama 24 lakini wakiwa wamecheza mechi moja zaidi ya Simba inayoshika nafasi ya nne pia ikiwa na alama 24

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
46m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’