Jana Azam Fc ilishindwa kuondoka na alama zote tatu mkoani Mbeya baada ya kulazimishwa suluhu ya bila kufungana dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo wa ligi kuu ya NBC.
Wakati Kocha wa Tanzania Prisons Shadrack Nsajigwa akifurahia alama hiyo moja, Florent Ibenge wa Azam Fc amelalamika timu yake kukosa matokeo kwa sababu ya ubovu wa uwanja wa Sokoine.





