Local,Normal News,Yanga, Simba

Yanga yahoji kanuni iliyotumika kumfungia mshambuliaji Simba

Joel JJ By Joel JJ
7 Mar 2026
Yanga yahoji kanuni iliyotumika kumfungia mshambuliaji Simba

Klabu ya Yanga imewaandikia barua kw Bodi ya Ligi, ikihitji ufafanuzi wa kina juu ya adhabu iliyotolewa na Kamati ya saa 72 kwa mchezaji wa Simba Selemani Mwalimu.

Akizungumza ktika mkutano na wanahabari mapema leo Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe alisema kuwa klabu hiyo imewasilisha barua rasmi baada ya kubaini kile walichokiita kuwa ni utofauti wa kikanuni katika kushughulikia makosa yanayofanana.

Kamwe amebainisha kuwa, wakati wachezaji wengine watano msimu huu walifungiwa mechi tano kwa makosa ya aina hiyo chini ya kanuni ya 41:21, Mwalimu amepewa adhabu ya mechi tatu pekee kwa kutumia kanuni ya 41:5(5.2).

Yanga imeitaka Bodi iweke wazi 'upekee' wa tukio la mchezaji huyo ulioifanya Kamati ya saa 72 kulegeza adhabu hiyo tofauti na msimamo uliochukuliwa kwa wachezaji wengine waliotangulia.

“Tumewaandikia barua Bodi ya Ligi, tukihitaji kupata ufafanuzi wa kina juu ya adhabu iliyotolewa na Kamati ya saa 72 kwa mchezaji Selemani Mwalimu. Msimu huu wachezaji watano wamefungiwa mechi 5 kwa kosa linalofanana na Mwalimu, lakini yeye amefungiwa mechi 3."

"Tunahitaji Bodi iweke bayana kuna upekee gani wa tukio la Mwalimu lililoifanya Kamati ya saa 72 kutumia kanuni tofauti ya 41:5(5.2) na wengine watano kutumika kanuni ya 41:21.”

“Jambo la pili, tumeitaka Bodi ya Ligi itoe ufafanuzi kwanini kamati ya saa 72 ilichelewa kukutana kama kanuni zinavyoelekeza ili kufanya mapitio ya makosa mbalimbali na kutoa hukumu kwa waliobainika ikiwemo tukio la mchezaji Selemani Mwalimu."

"Aidha mechi zingine zilizopita Kamati hii ya saa 72 ilikutana kwa wakati na kutoa hukumu. Kulikuwa na changamoto gani iliyopelekea kucheleweshwa kwa haki,”alisema Kamwe

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE →
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE →
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE →
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE →
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE →
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE →
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE →
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE →
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE →
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE →