International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumapili March 08 2026

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 Mar 2026
Tetesi za usajili Ulaya, Jumapili March 08 2026

Manchester United imemuongeza kiungo wa Bournemouth, Muingereza Marcus Tavernier, 26, kwenye orodha ya wachezaji inaowawinda. (Mail Plus - subscription required).

Unai Emery anaonekana kuwa na uwezekano mkubwa wa kuondoka Aston Villa msimu huu wa joto huku changamoto ya kocha huyo wa Uhispania ikiongezeka kutokana na vikwazo vya kifedha vinavyoizunguka klabu hiyo. (Football Insider)

Kutafuta kipa mpya nambari moja kwa Newcastle United kutakuwa muhimu kwa kocha Eddie Howe kwani kiwango cha Nick Pope kimedorora na Magpies hawataki kufanya uhamisho wa mkopo wa Aaron Ramsdale kutoka Southampton kuwa wa kudumu. (The Athletic - subscription required)

Mwakilishi wa meneja wa zamani wa Liverpool, Jurgen Klopp, anasema "kinachosemwa kuhusu mazungumzo ya kuifundisha Real Madrid ni uvumi tu kwa sasa" na kwamba "hakuna mtu aliyewasiliana nasi kwa sasa". (Goal)

Fabian Schar na Kieran Trippier ni wachezaji wengine wawili wa Newcastle ambao mustakabali wao haujulikani kwani klabu hiyo inakabiliwa na uwezekano wa kukosa kushiriki katika mashindano ya Ulaya msimu ujao. (ChronicleLive)

Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola, amehakikisha kuwa timu yake itakuwa bora zaidi msimu ujao, akidokeza kwamba ataheshimu mwaka wa mwisho wa mkataba wake kufuatia uvumi kwamba msimu huu unaweza kuwa wa mwisho kwa Mhispania huyo. (Sky Sports)

Mchezaji wa kimataifa wa Ureno Bernardo Silva, 31, anatarajiwa kuondoka Manchester City mwezi Juni kama mchezaji huru kwani hakuna mazungumzo yanayoendelea ya kurefusha mkataba wa kiungo huyo. (Matteo Moretto - in Spanish)

Edu ataacha wadhifa wake kama kiongozi wa soka huko Nottingham Forest miezi minane tu baada ya kuteuliwa, huku masharti ya kuondoka kwa Mbrazili huyo yakikamilishwa. (Talksport)

Liverpool wanaimarisha nia yao ya kumsajili mlinzi wa Nottingham Forest, Murillo na wanaamini pauni milioni 70 zinaweza kumsajili mchezaji huyo wa Brazil mwenye umri wa miaka 23. (Fichajes - in Spanish)

Manchester City wana nia ya kumsajili tena Felix Nmecha kama mbadala wa Elliot Anderson. Kiungo huyo wa kati wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 25 amevutia Borussia Dortmund msimu huu. (Football Insider)

Arsenal wanajiandaa kushinikiza uhamisho wa majira ya joto kwa kiungo wa Newcastle United Sandro Tonali, huku Manchester City na Manchester United pia wakimtaka mchezaji huyo wa kimataifa wa Italia mwenye umri wa miaka 25. (Tuttosport - in Italian)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’