Nsajigwa aipigia hesabu kali Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 8th March 2026


Nsajigwa aipigia hesabu kali Yanga

Kocha Mkuu wa Tanzania Prisons Shadrack Nsajigwa amesema malengo ya kikosi chake ni kuhakikisha wanaendelea kufanya vyema kwenye ligi kuu ya NBC ili kujiepusha na hatari ya kuteremka daraja.

Nsajigwa alianza vyema majukumu yake ya kuinoa Prisons akifanikiwa kuondoka na alama moja katika mchezo uliopita wa ligi kuu dhidi ya Azam Fc.

Mchezo unaofuata kwa Prisons ni dhidi ya mabingwa watetezi Yanga ambao watakutana nao Alhamisi, March 12 katika uwanja wa Sokoine.

Nsajigwa aliyewahi kuwa na nahodha wa Yanga, amesema kuelekea mchezo huo wanatambua ugumu ulio mbele yao lakini dhamira yake ni kuona kikosi chake hakipotezi mchezo huo.

"Tunajua ugumu wa Yanga, ni timu kubwa na wachezaji wazuri, lakini tunaenda mechi kwa mechi. Kila mchezo kwetu ni vita ya pointi ili tujiweke salama kwenye msimamo," alisema Nsajigwa

Kabla ya mchezo dhidi ya Yanga, Tanzania Prisons leo watashuka dimbani wilayani Chunya kuvaana na TMA katika Kombe la Shirikisho la CRDB (Hatua ya 32 bora).

Yanga pia itashuka dimba la KMC Complex kuikabili Polisi Tanzania kwenye mchezo wa kombe la CRDB


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.