Klabu ya Simba imethibitisha kumuongezea mkataba kiungo wa kati Yusuph Kagoma.
Kagoma ameongeza mkataba wa miaka miwili kuwatumikia Wekundu hao wa Msimbazi. Mkataba wake awali ulikuwa unamalizika mwishoni mwa msimu.
Ni hatua ya nzuri kwa uongozi wa Simba kumuongezea mkataba mapema kiungo huyo mkabaji ambaye kwa sasa ni moja ya nguzo ya Simba katika eneo la kiungo.





