Yanga yaifumua Polisi Tanzania 7-1 kombe la CRDB

Joel JJ By Joel JJ β€’ 8th March 2026


Yanga yaifumua Polisi Tanzania 7-1 kombe la CRDB

Yanga imetinga hatua ya 16 bora ya kombe la CRDB kibabe wakiibuka na ushindi wa mabao 7-1 dhidi ya Polisi Tanzania katika mchezo uliopigwa uwanja wa KMC Complex.

Zilikuwa dakika 90 ngumu kwa Polisi Tanzania mbele ya Wananchi waliokuwa na uchu wa kutinga hatua inayofuata ya michuano hiyo.

Mapema tu dakika ya kwanza Mudathir Yahya akaitanguliza kwa bao la shuti la chini chini kutoka nje kidogo ya 18.

Yanga iliendelea kutawala mchezo huo na kuongeza mabao zaidi kupitia kwa Depu aliyefunga 'hat-trik', Buba, Casemiro na Joseph Majagi aliyejifunga katika jitihada za kuokoa mpira uliopigwa na Okello ambao ulikuwa ukielekea wavuni.

Bao pekee la Polisi Tanzania lilikuwa la kujifunga beki wa Yanga Frank Assink katika jitihada za kuokoa mpira wa kona kwenye dakika ya 81.


>>> XTRA 90 MEDIA imetangaza nafasi za kazi. BONYEZA HAPA


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.