Kikosi cha Simba kimeondoka jijini Dar es salaam leo Jumatatu, March 09 kuelekea Singida tayari kwa mchezo wa ligi kuu dhidi ya Singida Black Stars.
Mchezo huo wa kwanza kuzikutanisha timu hizo msimu huu, utapiigwa Jumatano, March 11 katika uwanja wa Airtel, Mtipa.
Simba inatarajiwa kuweka kambi ya siku moja mkoani Dodoma kabla ya kuelekea Singida mapema Jumanne.





